JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

SHIRIKA LA POSTA TANZANIA


 

 

BODI YA WAKURUGENZI WA SHIRIKA LA POSTA TANZANIA

Brigedia Jenerali Mstaafu, Yohana Ocholla Mabongo

Mwenyekiti wa Bodi

 

Brigedia Jenerali Mstaafu Yohana Ocholla Mabongo ni Afisa Jenerali Mwanajeshi Mstaafu aliyezaliwa tarehe 10 Novemba 1958 Butimba Mkoani Mwanza. Yeye ni mzaliwa wa pili kati ya wana wanne na binti watatu wa Bw Richard Ocholla Mabongo na Lydia Miko Gorio. Alisoma Shule ya Msingi Masonga Wilayani Rorya hadi mwaka 1974 alipojiunga na Shule ya Sekondari ya Wavulana Tabora kuanzia mwaka 1975 hadi Februari 1981 na kumaliza masomo yake ya kidato cha sita.

Juni 1981 kwa mujibu wa sheria alijiunga na Jeshi la Kujenga Taifa Ruvu JKT na miezi sita baadaye aliandikishwa kujiunga na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania Januari 1982. Mara tu baada ya kuajiunga na Jeshi, Februari 1982 alichaguliwa kuendelea na kozi ya uhandisi katika Chuo cha Ufundi cha Kijeshi huko Cairo Misri, na kuhitimu mwaka 1986 katika Shahada ya Kwanza ya Uhandisi (B.Sc. Engineering).

Mwaka 1987 Brigedia Jenerali mstaafu Yohana alijiunga na kozi ya Maafisa Wanafunzi katika Chuo cha Jeshi la Tanzania (Tanzania Military Academy) na kutunukiwa cheo cha Luteni Usu, na punde tu siku hiyo hiyo Luteni na kupelekwa katika Kikosi cha Jeshi la Anga kama Mkuu wa Patuni na kushika nyadhifa mbalimbali kama Mhandisi wa Mawasiliano wa Kikosi, Afisa Mawasiliano wa Kikosi, na Mkufunzi katika shule ya Kikosi. Kufuatia kuchaguliwa kujiunga na Shule ya Mawasiliano ya Kijeshi na Chuo cha Anga cha Kijeshi na kufaulu vizuri Brigedia Jenerali alipandishwa cheo na kuwa Meja na kupewa uhamisho kwenda Chuo cha Mawasiliano ya Kijeshi mnamo mwaka 2001 kuwa Mkufunzi na Msaidizi Mkufunzi Mkuu.

Mnamo Oktoba 2001 Brigedia Jenerali Mstaafu Mabongo alihudhuria kozi ya Ukamanda na Unadhimu na baada ya kuhitimu 2002 alifanya kazi kama Afisa Mnadhimu wa Mawasiliano katika Makao Makuu ya Jeshi la Ulinzi  na baadaye mwaka huo huo 2002 aliteuliwa kuwa Msaidizi wa Mwajiri Mkuu (Personal Assistant) hadi 2006 alipopandishwa cheo kuwa Luteni Kanali na mwaka mmoja baadaye aliteuliwa kuwa Mkuu wa Kikosi katika Kikosi cha Mawasilianio (191) Wilaya ya Kisarawe hadi Oktoba 2008. Alipopandishwa cheo kuwa Kanali.

Mwaka 2008 baada ya kuanzishwa kwa Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu, Brig Jenerali mstaafu Mabongo alipandishwa cheo kuwa Kanali na kuteuliwa kuwa Afisa Mnadhimu Mawasiliano, Makao Makuu ya Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu hadi 2015 alipopandishwa cheo kuwa Brigedia Jenerali, na Februari 2016 aliteuliwa kuwa Katibu wa Chuo katika Chuo cha Taifa cha Ulinzi. Alihudumu kwa wadhifa huo hadi Julai 26, 2017 alipoteuliwa kuwa Mkuu wa Idara ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano katika Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, nafasi aliyoishikilia hadi alipostaafu tarehe 30 Juni 2018.

Brigedia Jenerali Mstaafu Mabongo, ni mhandisi aliyesajiliwa na Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB) na Mwanachama wa Chama cha Wahandisi Tanzania (MIET). Pia ana Shahada ya Uzamili katika Uhandisi wa Umeme kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (1996) na Mafunzo ya Usalama kutoka Chuo cha Taifa cha Ulinzi Tanzania (2014).

Brigedia Jenerali mstaafu amefanya safari nyingi za kimafunzo akiwa mwanafunzi na Mkufunzi katika Chuo cha Taifa cha Ulinzi katika nchi mbalimbali zikiwemo; Afrika Kusini, Namibia, Botswana, Ethiopia, Zambia, Bangladesh, India, China, Vietnam, Denmark na Sweden. Safari hizi za kimafunzo zimempa fursa ya kuwa na uzoefu na ufahamu wa kutosha kwa kutaja machache katika nyanja za uongozi na utawala, usalama na mafunzo ya kimkakati, uhusiano wa kimataifa itifaki, na diplomasia. Tuzo alizowahi kupata ni pamoja na Medali Iliyotukuka, Medali ya Utumishi wa Muda Mrefu, Medali ya Kagera, Medali ya Miaka 40 ya Jeshi na Medali ya Miaka 20 ya Jeshi.

           Ramadhan Omar Mohamed

                     Makamu Mwenyekiti wa Bodi

 

Bw. Ramadhan Omar Mohamed ni mjumbe wa ‘Mpango wa Marekebisho’ kutoka IMO Audit Zanzibar kwa kipindi cha miaka 5. Bw. Ramadhan Omar Mohamed ni msomi mwenye Shahada ya Uzamili ya Sheria kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Shahada ya Kwanza Sheria na ‘Sharia’ kutoka Chuo Kikuu cha Zanzibar, Stashahada na Cheti cha Elimu kutoka Taasisi ya Kiswahili na Lugha za Kigeni (Zanzibar). Bwana Ramadhan ana uzoefu wa zaidi ya miaka 6 katika fani ya Sheria huku akihudhuria kozi mbalimbali na warsha kutoka Taasisi ya ‘Intelijensia ya Kimataifa ya Sheria’ (ILI) –Zanzibar. Aidha Bw. Ramadhan Omar Mohamed amehudhuria Kozi ya Uandishi wa Sheria za mahakama na uhamiaji (Dar es Salaam). Ramadhan Omar Mohamed sasa ni Mjumbe wa Bodi ya Baraza la Uuguzi, Shirika la Utangazaji Zanzibar (ZBC) na Mjumbe wa Bodi ya Zabuni ya MOICT, Zanzibar.

Neema Mwalimu Mwanga

Mjumbe wa Bodi

Neema Mwalimu Mwanga ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Mkurugenzi wa Maliasili kutoka Wizara ya Katiba na Sheria. Bi. Neema Mwanga ni mzoefu katika masuala ya upelelezi, uhalifu wa kifedha wa kimataifa, na uhalifu wa mtandao kwa zaidi ya miaka 16 katika Jeshi la Polisi. Bi. Neema Mwanga ni mzoefu katika uratibu na usimamizi wa Mashirika yasiyo ya kiserikali yaliyo chini ya Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto. Kwa sasa anafanya kazi katika Wizara ya Katiba na Sheria kama Mkurugenzi wa Maliasili..Bi Neema ana Stashahada ya Uzamili ya Uongozi kutoka Chuo Kikuu cha Aalto (Finland), Stashahada ya Uzamili ya Uongozi na Uhusiano wa Kimataifa kutoka Chuo cha Diplomasia cha Tanzania na Msumbiji (Dar es Salaam –Tanzania), Shahada ya Sheria (LLB) kutoka Chuo Kikuu cha Dar es. Salaam, Diploma ya Sheria kutoka Chuo Kikuu cha Mzumbe, Cheti cha Sheria kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Cheti cha kozi za Polisi, Sheria za Trafiki kutoka Chuo cha Mafunzo ya Polisi Tanzania. Bi Neema Mwalimu Mwanga ameshika nafasi mbalimbali za kikazi ikiwemo msimamizi wa masuala ya Jinsia, Wazee na Watoto kutoka Wizara ya Afya, Mshauri Mkuu wa kisheria, utafiti na ushughulikiaji wa malalamiko kutoka Jeshi la Polisi Tanzania. Mkufunzi Mkuu kutoka Chuo cha Polisi Dar es Salaam, Kamanda wa Polisi Mkoa (Mkoa wa Mtwara), Afisa Utumishi/ Afisa Tawala (Mkoa wa Kipolisi Kinondoni) na Mshauri wa Masuala ya Kipolisi kutoka Umoja wa Mataifa (UNpol).

 

Dkt. Albogast Kilangi Musabila

Mjumbe wa Bodi

Dkt. Albogast Kilangi Musabila ni Mkurugenzi wa huduma za maktaba na ufundi (DLTS) kutoka Chuo Kikuu cha Mzumbe Tanzania ambako ana uzoefu wa zaidi ya miaka thelathini katika ngazi ya mhadhiri na Uongozi. Dkt. Albogast Kilangi ana Shahada ya Uzamivu ya Teknolojia ya Habari kutoka Chuo Kikuu cha VU(Netherlands ), Shahada ya Uzamili ya mifumo ya habari naTeknolojia kutoka Chuo Kikuu cha Agder (Norway), astashahada ya Mifumo ya Habari na Shahada ya Uzamili ya Usimamizi wa Biashara (Siviløkonom) kutoka Chuo Kikuu cha Agder University (Norway. Aidha Dkt. Albogast Kilangi Musabila and Diploma ya Usimamizi wa vifaa kutoka Chuo cha Mzumbe, Tanzania. Dkt. Albogast Kilangi Musabila ni Mshauri, Mtafiti na Mwandishi wa machapisho kadhaa ya Kitaaluma Tanzania.

 

 

 Andulile Jackson Mwakalyelye

Mjumbe wa Bodi

Bwana Andulile Jackson Mwakalyelye ni Mshauri Mwandamizi na mchumi mwenye uzoefu wa zaidi ya miaka 25 katika Benki na Fedha. Ana Shahada ya Uzamili katika Uchumi (Macroeconomics/Econometrics) na Shahada ya Kwanza katika Uchumi Usimamizi wa Fedha na Maendeleo ya Viwanda kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Ameshika nyadhifa za juu katika Benki mbalimbali nchini Tanzania, ikiwa ni pamoja na Makamu Rais wa Makazi na Mkuu wa kitengo cha Risk katika Bank ya Citibank, Mkuu wa Nchi wa Mikopo katika Benki za Stanbic na NMB, Mkuu wa Nchi katika Benki ya Maendeleo ya Afrika Mashariki, na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Azania. Andulile pia kwa sasa ni Mjumbe wa Bodi ya Citibank Tanzania na hapo awali amehudumu katika Bodi za Dar es Salaam Stock Exchange Plc (DSE), Benki ya Azania Limited, na Kampuni ya Urefushaji Mikopo ya Tanzania (TMRC). Pia amehudumu kama Mchumi wa Kitaifa kwa UNDP nchini Tanzania.

 

Chobo Paul Seleli

Mjumbe wa Bodi

Bw. Chobo Seleli ni Mkaguzi wa ndani wa Benki Kuu ya Tanzania (Tawi la Mbeya). Ni Mhasibu wa Umma Aliyeidhinishwa mwenye Astashahada ya Uhasibu kutoka Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) na Cheti cha Usuluhishi wa mambo ya kibenki cha cha Serikali ya Tanzania. Chobo Seleli alishika nyadhifa nyingine kama vile Mjumbe wa Baraza la Uongozi la Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE 2006-2007), Mkaguzi Mkuu wa Benki kutoka Benki Kuu ya Tanzania, Mkaguzi Msaidizi, Hazina Ndogo Wizara ya Fedha (MOF)-Mtwara. na Katibu wa Kampuni ya Mshauri wa Sayansi ya Jiolojia (GeSCO).

MESHACK JORAM ANYINGISYE

                                                                                                        Mjumbe wa Bodi

Meshack Joram Anyingisye is ni Mtaalamu wa Uchumi na Fedha mwenye cheo cha Kamishna wa Bajeti ya Serikali kutoka Wizara ya Fedha na Mipango. Meshack Joram Anyingisye ana Shahada ya Uzamili katika Usimamizi wa Miundombinu kutoka Chuo Kikuu cha Yokohama National University Mphil. Yokohama. Aidha Meshack Joram Anyingisye ana Shahada ya Uzamili katika Uchumi kutoka Chuo Kikuu cha Manchester Uingereza na Shahada ya Uchumi kutoka Chuo Kikuu cha Mzumbe. Aidha Meshack ana Astashahada ya ya uongozi kutoka Uongozi Institute na Chuo cha Alto, Finland.  Bwana Meshack Joram amefanya kazi kama Mchumi mbobezi katika Taasisi kadhaa ikiwemo, Benki ya Mendeleo Afrika, Ofisi ya Katibu Tawala Tanga na Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Vijijini.

 

 

 

 

Rudi Juu

© SHIRIKA LA POSTA TANZANIA