Habari
HERI YA SIKU YA MAMA DUNIANI

Leo, Shirika la Posta Tanzania linaungana na dunia nzima katika kuadhimisha *Siku ya Mama Duniani*, tukitambua mchango mkubwa, wa kipekee na usio na kifani wa mama katika familia, jamii na maendeleo ya taifa kwa ujumla.
Katika siku hii maalum, Shirika la Posta Tanzania linatuma salamu za pongezi kwa mama wote nchini kwa kazi kubwa wanayoifanya kila siku. Tukiwa kama shirika la huduma za jamii, tutaendelea kushirikiana na wanawake na mama katika kuhakikisha huduma bora na jumuishi zinapatikana kwa wote.